Matthew 15

1Ndipo Mafarisayo na waadishi walikuja kwa Yesu kutoka Yerusalemu. Na kusema, 2“Kwa nini wanafunzi wanayahalifu mapokeo ya wazee? Kwa kuwa hawanawi mikono yao wanapokuwa wanakula chakula.‘’ 3Yesu akawajibu na kuwaambia, “Nanyi__kwa nini mnaihalifu sheria ya Bwana kwa ajili ya mapokeo yenu?

4Kwa kuwa Mungu alisema, ‘Mheshimu baba yako na mama yako; na ‘Asemaye uovu kwa baba yake na mama yake, hakika atakufa.’ 5Lakini ninyi husema, ‘Kila amwambiaye baba yake na mama yake, ‘”Kila msaada ambao angepata kutoka kwangu sasa ni zawadi kutoka kwa Mungu,‘‘’ 6“Mtu huyo hana haja ya kumuheshimu baba yake. Katika namna hii mmelitangua neno la Mungu kwa ajili ya mapokeo yenu.

7Enyi wanafiki, ni vema kama Isaya alivyo tabiri juu yenu aliposema, 8‘Watu hawa wananiheshimu mimi kwa midomo yao, lakini mioyo yao iko mbali nami. 9Wananiabudu bure, kwa sababu wanafundisha mafundisho yaliyo maagizo ya wanadamu.”’

10Ndipo akawaita makutano na kuwaambia,” Sikilizeni na mfahamu__ 11Hakuna kitu kiingiacho mdomoni mwa mtu na kumfanya najisi. Bali, kile kitokacho kinywani, hiki ndicho kimfanyacho mtu kuwa najisi.‘’

12Ndipo wanafunzi wakamwendea na kusema na Yesu, “Je!, Unafahamu Mafarisayo walipolisikia lile neno walikwazika?” 13Yesu aliwajibu na kusema, “Kila mmea ambao Baba yangu wa mbinguni hajaupanda utang’olewa. 14Waacheni pekee, wao ni viongozi vipofu. Kama mtu kipofu atamuongoza kipofu mwenzake, wote wawili wataanguka shimoni.”

15Petro akajibu na kumwambia Yesu,” Tuelezee mfano huu kwetu, 16Yesu akajibu, ‘’Nanyi pia bado hamuelewi? 17Ninyi hamuoni kuwa kila kiendacho mdomoni hupitia tumboni na kwenda chooni?.

18Lakini vitu vyote vitokavyo mdomoni hutoka ndani ya moyo. Ndivyo vitu vimtiavyo mtu unajisi. 19Kwa kuwa katika moyo hutoka mawazo mabaya, uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo, na matusi. 20Haya ndiyo mambo yamtiayo mtu unajisi. Lakini kula bila kunawa mikono hakumfanyi mtu kuwa najisi.”

21Ndipo Yesu akatoka mahali pale na akajitenga kuelekea pande za miji ya Tiro na Sidoni. 22Tazama akaja mwanamke Mkanani kutoka pande hizo. Akapaza sauti akisema, ‘’Nihurumie, Bwana, Mwana wa Daudi; binti yangu anateswa sana na pepo.‘’ 23Lakini Yesu hakumjibu neno. Wanafunzi wake wakaja wakimsihi, wakisema, ‘’Muondoe aende zake, maana anatupigia kelele.‘’

24Yesu aliwajibu na kusema, Sikutumwa kwa mtu yeyoye isipokuwa kwa kondoo waliopotea wa nyumba ya Israeli.‘’ 25Lakini alikuja na kuinama mbele yake, akisema, ‘’Bwana nisaidie.‘’ 26Alimjibu na kusema, “Siyo vema kuchukua chakula cha watoto na kuwatupia mbwa,”

27Akasema, “Ndiyo, Bwana, hata hivyo mbwa wadogo hula chakula kiagukacho mezani mwa Bwana wao.” 28Ndipo Yesu akajibu na akisema “Mwanamke, imani yako ni kubwa. Na ifanyike kwako kama utakavyo.” Na binti yake alikuwa ameponywa katika wakati huo.

29Yesu aliondoka mahali pale na kwenda karibu na bahari ya Galilaya. Kisha alienda juu ya mlima na kuketi huko. 30Kundi kubwa likaja kwake. Na kumletea viwete, vipofu, bubu, vilema na wengine wengi, waliokuwa wagonjwa. Waliwaweka katika miguu ya Yesu na akawaponya. 31Nao umati wakashangaa walipoona mabubu wakiongea, na vilema wakifanywa wazima, viwete wakitembea, na vipofu wakiona. Walimsifu Mungu wa Israeli.

32Yesu akawaita wanafunzi wake na kusema, “Nimewaonea huruma umati, kwa sababu wamekuwa nami kwa siku tatu bila kula kitu chochote. Sitawaaga waende kwao bila kula, wasije wakazimia njiani.” 33Wanafunzi wake wakamwambia, “Ni wapi tunaweza kupata mikate ya kutosha hapa nyikani kushibisha umati mkuwbwa hivi?” 34Yesu akawaambia, “Mna mikate mingapi?” Wakasema, “Saba, na samaki wadogo wachache.” 35Yesu akawaamuru umati uketi chini.

36Aliitwaa ile mikate saba na samaki, na baada ya kushukuru, akaimega na kuwapa wanafunzi. Wanafunzi wakawapa umati. 37Watu wote wakala na kutosheka. Na wakakusanya mabaki ya vipande vya chakula vilivyosalia vipande vipande, vilijaa vikapu saba. 38Wote waliokula walikuwa wanaume elfu nne bila wanawake na watoto. Kisha Yesu akauaga umati waende zao na akaingia ndani ya mashua na kwenda sehemu za Magadani.

39

Copyright information for SwaULB